Genesis 10:1-6

Mataifa Yaliyotokana Na Nuhu

(1 Nyakati 1:5-23)

1 aHawa ndio wazao wa Nuhu: Shemu, Hamu na Yafethi, ambao walizaa wana baada ya gharika.

Wazao Wa Yafethi


2 bWana wa Yafethi walikuwa:
Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Mesheki na Tirasi.

3 cWana wa Gomeri walikuwa:
Ashkenazi, Rifathi na Togarma.

4 dWana wa Yavani walikuwa:
Al-Yasa, Tarshishi, Kitimu na Rodanimu.
5(Kutokana na hawa mataifa ya Pwani yalienea katika nchi zao, kwa koo zao katika mataifa yao, kila moja kwa lugha yake.)

Wazao Wa Hamu


6 eWana wa Hamu walikuwa:
Kushi, Misri,
Yaani Misri .
Putu na Kanaani.
Copyright information for SwhKC